CRM LAND CONSULT (T) LTD YAONGOZA UPANGAJI MIJI TANZANIA: Yapokelewa kwa vifijo na ndelemo wilayani Gairo



PROGRAMU YA KUPANGA, KUPIMA NA KUMILIKISHA ARDHI GAIRO MJINI





IMEANDALIWA NA KUWASILISHWA
NA
ISMAIL R. CHINGWELE
MTAALAM MSHAURI WA MIPANGO MIJI NA ARDHI
CRM LAND CONSULT (T) LTD
DAR ES SALAAM-TANZANIA


1.0  Utangulizi
Tanzania inakabiliwa na ongezeko kubwa la watu na mahitaji ya ardhi kwa matumizi mbalimbali ya kiuchumi na kijamii.
Ukuaji wa kasi wa miji usiozingatia mpangilio wa mipango miji pamoja na kuongezeka kwa kasi kwa ujenzi holela kumesababisha kuwa na makazi yasiyo na huduma muhimu za kijamii pamoja na miundombinu na mazingira yasiyo safi na salama kiafya, ambayo, pamoja na mambo mengine, husababisha magonjwa ya milipuko. Pia ujenzi holela huikosesha Serikali mapato yatokanayo na kodi za ardhi.
Aidha, kutokuwepo kwa mpango wa matumizi ya ardhi katika maeneo ya vijijini, hususan yanayotenganisha maeneo ya malisho ya mifugo na kilimo, uvamizi na uanzishwaji holela wa mashamba, ni chanzo cha muingiliano wa matumizi ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji. Hali kama hii hutokea pia kati ya wakulima na wawekezaji, Serikali za Vijiji na Hifadhi za Taifa, vijiji na vijiji na wilaya na wilaya. Hali hii husababisha uvunjifu wa amani na hata kusababisha baadhi ya watu kupoteza maisha na mali zao.
Vilevile, kutofautiana kwa mipaka ya kiutawala inayotokana na Matangazo ya Serikali (GN), ramani za upimaji wa vijiji na ramani za Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012 kumechangia kuwepo kwa mpaka zaidi ya mmoja na hivyo kusababisha migogoro ya mipaka katika maeneo husika.
Sera ya Taifa ya Ardhi ya Mwaka 1995, inabainisha haki ya kila Mtanzania kumiliki ardhi nchini. Utekelezaji wa Sera hii unafanyika kwa kutumia Sheria ya Ardhi Na. 4 ya Mwaka 1999 na Sheria ya Ardhi ya Vijiji Na. 5 ya Mwaka 1999. Sheria nyingine ni Sheria ya Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi Na. 2 ya Mwaka 2002, Sheria Na. 6 ya Matumizi ya Ardhi ya Mwaka 2008 na Sheria Na. 8 ya Mipango Miji ya mwaka 2007.
Utekelezaji wa Sera na Sheria, pamoja na mambo mengine, unalenga kuhakikisha kwamba, elimu kuhusiana na Sheria hizi inatolewa na kuwafikia wananchi; mipaka ya Vijiji inapimwa; Vijiji vinaandaliwa Mipango ya Matumizi ya Ardhi; kila mji unaandaliwa Mpango wa Jumla unaotoa mwongozo wa ukuaji wa mji; viwanja katika maeneo mapya vinapimwa na kumilikishwa; maeneo yaliyoendelezwa kiholela yanarasimishwa na wananchi wanapatiwa hatimiliki zao; kila kipande cha ardhi kijijini kinapimwa na kumilikishwa; na migogoro ya ardhi baina ya watumiaji inatatuliwa.
Fursa zilizopo katika kutekeleza program hii ni pamoja na kuwapo kwa miradi mingine inayoendelea kutekelezwa inayofanana na progamu hii, utayari wa wananchi kupimiwa maeneo yao na kusuluhisha migogoro inayowakabili, pamoja na utayari wa Serikali kushirikiana na sekta binfsi katika utekelezaji wa Programu hii. Fursa nyingine ni kuwapo kwa wataalam wa kutekeleza kazi hii, utashi wa viongozi wa kisiasa kwa kushirikiana na Serikali na kuhakikisha wananchi wanapimiwa ardhi yao na kumaliza migogoro inayowakabili.
Katika kukabiliana na changamoto zilizopo katika sekta ya ardhi, hususan migogoro ya ardhi, Serikali imepanga kutekeleza Programu ya Kitaifa ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi, ili kwenda sambamba na mpango elekezi wa Taifa wa muda mrefu (2016/2017 – 2020/2021) ambapo sekta ya ardhi imepewa kipaumbele. Hata hivyo serikalin kwa kutambua ufinyu wa bajeti uliopo, iliazimia kushirikisha sekta binfsi katika utekelezaji wa programu hii.
Madhumuni ya Program hii ni kuhakikisha kuwa ardhi yote ya Tanzania inapangwa, kupimwa na kumilikishwa na kumbukumbu zake kuhifadhiwa, ili kuweka mazingira bora ya usimamizi wa ardhi.
Matokeo yanayotarajiwa kutokana na utekelezaji wa Programu hii, ni kuwa na mipaka sahihi katika ngazi zote za kiutawala (Vijiji na vitongoji ndani ya wilaya). Aidha, ardhi itakuwa imepangwa, na kila kipande cha ardhi kupimwa na kumilikishwa.  Utekelezaji huo utawezesha kuwa na usalama wa miliki, kuongezeka kwa thamani ya ardhi na maduhuli ya Serikali, kurahisishwa upatikanaji wa taarifa za ardhi, kuboreshwa kwa mazingira,  kupungua kwa migogoro ya ardhi na kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji.
1.1 Programu ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi Gairo
Mji wa gairo ni miongoni mwa miji inayo kua kwa kasi nchini na inakabiliwa na ongezeko kubwa la watu na Ujenzi holela hivyo kua na uhitaji wa kurasimishwa na kumilikishwa kwa wananchi ili halmashauri iongeze mapato yake kupitia kodi ya Ardhi na wananchi pia waweze kutanua wigo wa dhamana kiuchumi, kijamii na kisiasa kwa kutumia hatimiliki ya Ardhi watakayo kua nayo.
Maeneo yalio onekana kua na uhitaji mkubwa Zaidi ni yale ya katikati ya mji yaani CBD ambayo yanakabiliwa na Ujenzi na ongezeko kubwa la kazi mbalimbali za kiuchumi. maeneo haya yalionesha uhitaji mkubwa sana wa kupanga kupimwa na kumnilikishwa kwa wanachi na hii imetokana na ukuaji wa kasi wa kata hizi usiozingatia sheria za kitaalam za mipango miji ikiwemo sheria ya mipango miji ya mwaka 2007.
1.2 Hasara za makazi holela katika maendeleo ya mji
Moja ya hasara ya kuwepo kwa makazi holela ndani ya mji ni kusababisha ugumu wa utoaji huduma za jamii kwa wananchi wanao ishi maeneo hayo zikiwemo maji safi, maji taka, uhifadhi wa taka ngumu, elimu, afya na barabara, hasara nyinginezo ni pamoja na;-
  • Kutengeneza sura mbaya ya mji
  • Hatari ya milipuko ya magonjwa kutokana na ukosefu wa mifereji ya kupitishia maji taka na maji ya mvua wakati wa  mvua
  • Jamii kukosa dhamana ya kujikwamua kiuchumi na hivyo kupelekea ugumu wa maisha na hali ngumu ya kujikwamua na baa la umasikini
  • Serikali kukosa mapato yanayoweza kutokana na kodi ya Ardhi na hivyo kupelekea ufinyu wa majeti ya  kazi za kimaenddeleo ndani ya mji
  • Migogoro ya matumizi ya Ardhi na mipaka ya viwanja baina ya wananchi. Mfano wa migogoro ya matumizi ya Ardhi hutokea pale kunapokua na muingiliano wa nyumba za ibada na makazi, kumbi za starehe na makazi. N.k
1.3 Njia za kutatua tatizo la makazi holela Gairo
Kupitia sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999 na ile ya mipango miji namba 8 ya mwaka 2007 inaelekeza namna ya kutatua tatizo la makazi holela nchini kua ni kurasimisha na kumilikisha maeneo hayo kwa kupanga, kupima na kutoa hatimiliki za viwanja katika eneo husika, pia kuzingatia kutoa maneneo ya huduma ndani ya eneo hilo kama vile maeneo ya shule na zahanati.
Lakini pia Urasimishaji wa makazi holela ulianishwa na kusisitizwa na waziri wa Ardhi nyumba na maenedelo ya makazi mwaka 2016 pale alipozitaka halmashauri zote nchini kushirikiana na sekta binafsi kurasimisha makazi holela ndani ya halmashauri zao kwa kutumia mbinu shirikishi.
Kupitia tamko hilo, andiko hili linalenga kuunga mkono juhudi za serikali za kutaka kupanga, kupima na kumilikisha kila kipande cha Ardhi nchi nzima pia kuunga mkono juhudi za waziri wa Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi zinazo lenga kutoa hati za kumiliki Ardhi 400,000 kwa mwaka.
Kukamilika kwa miradi ya urasimishaji ndani ya mji wa Gairo kutakua na faida zifuatazo;-
  • Kudhibiti Ukuaji wa maendeleo holela unaoharibu sura ya mji
  • Kudhibiti kuongezeka kwa idadi ya migogoro miongoni mwa watumiaji wa ardhi.
  • Kuwa na uhakika wa miliki na matumizi ya Ardhi katika eneo husika.
  •  Kuimarisha soko la ardhi lisilo rasmi linalo fanywa na wananchi ndani ya mji na hivyo kuwainua kiuchumi wananchi wa hali ya chini wanaotegemea Ardhi kama sehemu ya kujikwamua kimaisha.
  • Kupunguza hatari ya milipuko ya magonjwa ndani ya maeneo husika kwa kutenga maneneo ya taka na ifereji ya kusafirishia maji taka na maji ya mvua.
  • Kuweka utaratibu wa matumzi bora ya rasilimali ardhi kwa kutatua migogoro, hasa ya mipaka ya viwanja.
  • Kuimarisha miliki za ardhi na matumizi yake kwa kuainisha thamani ya miliki hizo katika maisha ya kila siku ya mtu mmoja Mmoja na mji kwa ujumla.
  • Kuboresha matumizi na hifadhi ya ardhi kulingana na mapendekezo na uwezo wa walengwa.
  • Kuboresha hali ya maisha ya watu kuondoa umasikini na utunzaji wa mazingira ndani ya mji.
Hata hivyo faida hizo zimegawanywa katika makundi manne kama ifuatavyo;-



2.0  Faida za Programu Gairo

Utekelezaji wa Programu ya kupanga, kupima na kumilikisha kila kipande cha ardhi nchini unalenga kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika sekta ya ardhi. Kazi hii inahitaji msukumo na ushirikishwaji wa wadau na jamii nzima unaozingatia misingi ya haki na demokrasia. Kazi zitakazotekelezwa katika Programu hii ni pamoja na uhamasishaji na utoaji wa elimu kwa umma, uhakiki wa michoro iliopo, uandaaji wa mipango  ya matumizi ya ardhi,  upimaji na umilikishaji wa kila kipande cha ardhi.
Utekelezaji wa Programu hii unatarajiwa kuleta matokeo chanya yatakayoleta faida za kijamii, kiuchumi, kimazingira na kiutawala kwa mtu mmoja mmoja, Taasisi na Taifa kwa ujumla.

2.1          Faida za Kiuchumi

Utekelezaji wa Programu hii utaongeza thamani ya ardhi na kuibadilisha kutoka mtaji mfu kuwa mtaji hai na hivyo kuifanya itoe mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi. Upimaji na umilikishwaji  wa vipande vya ardhi Mijini na vijijini utachangia ustawi wa nchi kupitia kodi ya pango la ardhi kwa wamiliki wa ardhi, kuongeza wigo wa uzalishaji mali kupitia biashara na mikopo itakayotolewa na vyombo vya fedha.
Hivyo, faida za kiuchumi zitakazopatikana baada ya Programu hii kutekelezwa ni pamoja na kuongezeka kwa maduhuli ya Serikali yatokanayo na ardhi; kuongezeka kwa shughuli za uzalishaji mali; kuongezeka kwa thamani ya ardhi na kuboreshwa kwa mazingira ya kufanyia biashara na shughuli za uwekezaji.

2.2          Faida za Kimazingira

Katika utekelezaji wa Programu hii, kila kipande cha ardhi kitapangiwa matumizi na kupimwa, hivyo ardhi yote ya Tanzania itakuwa na matumizi yanayojulikana na kuondoa mwingiliano wa matumizi.  Vilevile, mipango ya matumizi ya ardhi itasaidia ardhi yote kutunzwa na watumiaji husika na kuhifadhiwa kwa maliasili zilizopo na mazingira kwa ujumla. Pia, jamii inayozunguka maeneo yaliyohifadhiwa itawezeshwa kutambua mipaka yao na kuwa na mipango ya matumizi ya ardhi na kudhibiti uvamizi wa maeneo hayo.
Aidha, utekelezaji wa Programu hii utajenga uelewa wa jamii wa kutunza ardhi wanayomiliki dhidi ya uharibifu wowote; kuwezesha kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi; kuboresha makazi ya wananchi na kuleta usalama na ustawi wa maliasili za Taifa.

2.3          Faida za Kiutawala

Matokeo ya utekelezaji wa Programu hii ni kuwa na mipaka iliyohakikiwa, kurekebishwa na kuridhiwa na pande husika. Hali hii itawezesha kuondokana na migogoro ya mipaka na hivyo kuleta utulivu na amani katika jamii.
Mipaka isiyo na kasoro itawasaidia watawala kufahamu maeneo ya mamlaka yao kwa usahihi hivyo kuwawezesha kuratibu shughuli za usimamizi wa mipango mbalimbali. Aidha, itawasaidia wananchi kujua wanakowajibika kiutendaji na mahali wanapostahili kupata huduma mbalimbali kwa ajili ya shughuli za kijamii, kisiasa na kiuchumi.
Kazi ya usimamizi wa shughuli za maendeleo, ulinzi na usalama hufanyika ndani ya mipaka ya kiutawala inayofahamika hivyo utekelezaji wa programu hii utawezesha kuwepo na uwajibikaji na ufuatiliaji wa karibu.
Pia vilevile utekelezaji wa program hii utaisaidia serikali kupata faida za moja kwa moja kama vile kupimiwa maeneo yote ya taasisi( shule, zahanati, maeneo ya wazi na barabara za ndani) bure na kukabidhiwa mkurugenzi wa wilaya kwa niaba ya wananchi, kwa kufanya hivyo itasaidia utambuzi wa maeneo hayo na hivyo kudhibiti uvamizi wa wananchi katika maeneo hayo.
Kwa upande wa vijijini, baada ya uhamasishaji kukamilika na wananchi kujenga mwamko wa utekelezaji wa program hii, serikali pia kupitia halmashauri hii, itapata maeneo mapya kutoka kwa wananchi yatakayo weza kutumika kwa fidia ya maeneo ya umma

2.4          Faida za Kijamii

Kijamii, utekelezaji wa Programu utasaidia kutatua migogoro ya ardhi iliyopo baina ya watumiaji, kuzuia migogoro ya mipaka ya kiutawala, na hivyo kudumisha amani na utulivu katika jamii, na kuleta maelewano kati ya watumiaji mbalimbali wa ardhi
3.0  Eneo lililo athiriwa zaid na makazi holela gairo
Wilaya ya Gairo ni miongoni mwa wilaya zinazokua kwa kasi kubwa kulinganishwa na wilaya nyingine nchini. Wilaya hii ni miongoni mwa maeneo nchini yanayo kabiliwa na ongezeko kubwa la watu na shughuri za kiuchumi zinazo pelekea mahitaji ya Ardhi kuongezeka siku hadi siku. Miongoni mwa maeneo yalio athiriwa zaid wialayani Gairo ni pamoja na kata Gairo, Luhwaji, Majawanga, Ukwamani, Mkalama, Meshugi na Msingisi zote hizi zinapatikana ndani ya mamlaka ya mji mdogo wa Gairo.
Kijografia eneo hili linaonekana kuania ngazi ya taifa, mkoa, wilaya na mji mdogo kama invyoonekana katika ramani zifuatazo.
Kielelezo namba 1: Ramani ya Tanzania kuonesha mkoa wa Morogoro ambao ndani yake hupatikana wilaya ya gairo





Kielelezo namba 2: Ramani ya mkoa wa Morogoro kuonesha wilaya ya Gairo ambayo ndani yake hupatikana mji mdogo wa Gairo




Kielelezo namba 3: Ramani ya wilaya ya Gairo kuonesha mji mdogo wa Gairo ambayo ndani yake kuna kata zilizo athirika zaid



Kilelezo namba 4: Ramani ya mji mdogo wa Gairo kuonesha kata zenye maeneo yaliuo athirika kwa makazi holela
Hata hivyo kutoka kilelezo namba 4, ifuatayo ni picha ya anga kuonesha hali halisi ya kata ya Gairo ambayo ni miongoni mwa kata saba zilizo athirika zaid na makazi holela.



Kwa kawaida ardhi haiongezeki, licha ya kwamba idadi ya watu na shughuli juu ya ardhi zinaongezeka siku hadi siku. Tanzania, kama nchi nyingine zinazoendelea ina idadi kubwa ya watu inayofikia kiasi cha milioni 49 kwa maoteo ya mwaka 2017 yanayotokana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012.  Kasi ya ongezeko la idadi ya watu ni asilimia 2.7 kwa mwaka ambalo limesababisha mahitaji ya ardhi kwa matumizi mbalimbali ya kiuchumi na kijamii kuongezeka.
Ukuaji wa Miji midogo kuwa miji mikubwa na majiji umesababisha kuwepo kwa changamoto ya upatikanaji wa ardhi hususan ardhi iliyopangwa na kupimwa. Pia, kumekuwepo na ukuaji wa kasi wa miji ambao hauzingatii mpangilio wa mipango miji na kuongezeka kwa kasi kwa ujenzi holela wenye makazi yasiyo na huduma muhimu za kijamii pamoja na miundombinu na mazingira yasiyo safi na salama kiafya.
Katika maeneo ya vijijini, matumizi ya ardhi yamekuwa hayazingatii mpango wa matumizi ya ardhi, yanayotenganisha sehemu za malisho ya mifugo na kilimo, uvamizi wa maeneo yaliyohifadhiwa na uanzishwaji holela wa mashamba. Hali hii imesababisha uvunjifu wa amani na baadhi ya watu kupoteza maisha na mali zao.
Aidha, kutofautiana kwa mipaka ya kiutawala inayotokana na Matangazo ya Serikali (GN), ramani za upimaji wa vijiji na ramani za Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012 kumechangia kuwepo kwa mpaka zaidi ya mmoja na hivyo kusababisha migogoro ya mipaka katika maeneo mbalimbali nchini.
Programu hii ambayo itahusisha kupanga, kupima na kumilikisha ardhi vijijini na mijini itasaidia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa ardhi wakati wote kwa matumizi ya vizazi vyote na kuondoa migogoro ya ardhi katika jamii. Aidha, kuwa na ardhi iliyopangwa, kupimwa na kumilikishwa kunaongeza uhakika wa usalama wa milki, thamani ya ardhi na kuchangia kupunguza umaskini kwa kutumia kikamilifu fursa za matumizi ya ardhi hiyo kama dhamana ya mikopo kutoka katika taasisi za kifedha.
Vilevile, kuwa na mipaka sahihi ya kiutawala kunawezesha watawala kufahamu maeneo ya mamlaka yao kwa usahihi hivyo kuwasaidia katika kuratibu shughuli za usimamizi wa mipango mbalimbali ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.
Taarifa na takwimu zote zinazohusiana na matokeo ya utekelezaji wa Programu hii zitaingizwa katika Kanza ya Taifa ya takwimu za ardhi kwa ajili ya utunzaji wa kumbukumbu za ardhi. Kumbukumbu hizo zitakuwa msaada mkubwa katika kuainisha na kusimamia maeneo yote yaliyokwishapimwa. Pia, taarifa hizo zitatumika wakati wa utekelezaji wa programu mbalimbali za Kitaifa zikiwemo Sensa ya Watu na Makazi, vitambulisho vya makazi, anuani za makazi, masuala ya ulinzi na usalama wa nchi na programu nyingine zinazotekelezwa na Serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Hata hivyo kwa kutambua umuhimu wa pogramu hii kampuni ya CRM Land Consult (T) Ltd imedhamilia kushirikiana na serikali pamoja na wananchi kukamilisha program hii itakayo kua na faida kwa serikali na wananchi kwa ujumla.
Kampuni y CRM Land Consult (T) Ltd inalenga kufanya yafuatayo ili kuhakikisha programu inakua na faida kwa wilaya na viunga vyake;-
·         Kuunganisha wadau mbalimbali wa maendeleo ndani ya mji ili kuwezesha uungwaji mkono wa programu hii
·         Kuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi ili kujenga utayari wa kupangwa,kupimiwa na kumilikishwa maeneo yao
·         Kupanga na kutenga matumizi mbalimbali ya Ardhi katika vijiji vilivyo pembezoni mwa mji kwa kushirikiana na wananchi katika maeneo hayo.
Vile vile kampuni ya CRM Land Consult (T) Ltd ina nguvu kazi na vifaa vya teknolojia ya kisasa kuweza kufanya kazi hii kwa uharaka Zaidi na ina rasili mali watu wenye weredi mkubwa wenye uwezo wa kuhamasisha na kutoa elimu yenye kuzingatia sheria na sera zote za Ardhi kwa wananchi.
CRM Land Consult (T) Ltd imefanya kazi nyingi ndani ya nchi kama inavyoonekana katika wasifu wa kampuni uliombatanishwa na andiko hili (rejea wasifu wa kampuni).


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CRM LAND CONSULT (T) LTD IS A BEST FIRM IN LAND PLANNING AND MANAGEMENT IN TANZANIA